Vichwa vya Habari
Makala Maalum
Utamaduni na Elimu
Nchini Burkina Faso, ufadhili kutoka Mfuko wa Elimu Haiwezi Kusubiri au Education Cannot Wait, wadau wa elimu duniani likiwemo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF na wadau wa kimkakati wanawarejesha shuleni wasichana na wavulana. Wanarejeshwa maeneo salama wanakoweza kujifunza kwa njia mbali mbali ikiwemo kupitia vipindi vya redio. Wakipatiwa mafunzo kama ya ufundi ili hatimaye wajifunze kile walichokosa.
Habari kwa Picha
Harakati za kusaka usalama huko Gaza
Wengi wa wananchi wa Gaza milioni 2.3 wanakimbia ghasia zinazozidi kaskazini na Kusini mwa Gaza kutokana na vita ambayo sasa ina miezi saba na ambayo imesababisha vifo vya wapalestina 36,000 na kuwaacha wengine katika njaa huku wengine wakiwa wamefukiwa kwenye vifusi katika maeneo yaliyo zingirwa.
Habari Nyinginezo
Amani na Usalama
Mapigano makali yanayoendelea kaskazini mwa Gaza yamelazimu watu wapatao 84,000 kukimbia eneo la mashariki la mji wa Gaza ndani ya siku chache, huku mapigano hayo yakisababisha pia kukatika kwa mawasiliano na eneo muhimu linalohusika na usambazaji wa misaada, yamesema mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayotoa misaada ya kibinadamu eneo hilo.
Amani na Usalama
Afisa Mwandamizi wa jeshi la Sudan Kusini, Brigedia Jenerali Liep Bol Lam amewaomba wananchi wa Sudan Kusini kuungana pamoja ili kujenga taifa hilo.